kalimah.top
a b c d e f g h i j k l m n o p q r s t u v w x y z 0 1 2 3 4 5 6 7 8 9 #

sabah salum – hakuna jipya كلمات اغاني

Loading...

hakuna jipya taarab _ sabah salum

mkombozi records

hakuna ubaya mpya yoote ni yale yale
afanyalo jipya dunia ni ile ile
hakuna ubaya mpya yoote ni yale yale
afanyalo jipya dunia ni ile ile

upepo ukivuma kasi utakwenda kasikaziiii
neno ukigeuza tusi hauninyimi usingizi
upepo ukivuma kasi utakwenda kasikaziiii
ooohhhhhh
neno ukigeuza tusi hauninyimi usingiziii
ridhiki yangu sikosi na maneno hayaudhi
sinichafueni basi tunajaziana nzii
ooohhhhhh
ridhiki yangu sikosi na maneno hayaudhi
sinichafueni basi tukajaziana nzii

mapenzi ni yaleyale waliyoanza mababu jipya alitotokeaa
ubaya ni vile vile hayo mengine sababu waja mwanitafutiaa
mapenzi ni yaleyale waliyoanza mababu jipya alitotokeaa
ubaya ni vile vile hayo mengine sababu waja mwanitafutiaa
nao wema ni ule ule malipo yake thawabu mola alishatuambiaa
vyeema kuwa mpoole tusitiane ghadhabu siku kaniaribiaaa
nao wema ni ule ule malipo yake thawabu mola alishatuambiaa
vyeema kuwa mpoole tusitiane ghadhabu siku kaniaribiaaa
usininyooshee kidolee hutonitia aibuuu ooh tuli nitakuangalia
sina iridhi sina chale mlinzi w_ngu wahaabu oohhh yeye namtegemea
sininyooshee kidolee hutonitia aibuuu tuli nitakuangalia
sina iridhi sina chale mlinzi w_ngu wahaabu yeye namtegemea

likotoka mashariki magharibi litatuaa

kusanya na mashabiki waje mje muuze jua
likotoka mashariki magharibi litatuaa

kusanya na mashabiki waje mje muuze jua

kama hilo uliwezii basi yoote yaleyalee
hata mimi huniwezi mola kaniweka mbele
kama hilo uliwezii basi yoote yaleyalee
hata mimi huniwezi mola kaniweka mbele

ubaya toka zamani nilipokuwa mdogo
maneno yake kinywani komwe haliwi kisogo
ubaya toka zamani nilipokuwa mdogo
maneno yake kinywani komwe haliwi kisogo
alo kula amekula kala nini haijuzu
iwe biriani kala au dagaa kauzu
tuombeane sitara tusitenguane udhu
ubaya toka zamani nilipokuwa mdogo
maneno yake kinywani komwe haliwi kisogo
hakuna lililo jipya lipate kunish_tua
ambalo mtajitapa moyo mkanilipuaa
hakuna ubaya mpya ulio chini ya juaa
ubaya toka zamani nilipokuwa mdogo
maneno yake kinywani komwe haliwi kisogo

taarab/mshairi /lyrics

كلمات أغنية عشوائية

اهم الاغاني لهذا الاسبوع

Loading...