ksonrap – ndoto ya mchana كلمات اغاني
[intro]
this one right here is for the people
nimelala mchana nikaota
yeah, let’s go
[verse1: ksonrap]
ajira hakuna tunasuk_ma mikokoteni;
wanasiasa baada ya kampeni wameingia tu mitini;
bila hata kandili wametuacha tu gizani;
hakuna kufanya mikutano chama cha upinzani;
kila kitu wametupiga pini wanasingizia vita vya ukraine;
vitu vinapanda bei madukani nachokisema nikweli wala sio utani;
hali mbaya wafanya biashara wan_z_funga tu mizani;
shekhe msikitini anakosa hela yakununua hata ubani;
hakuna anaetoa sadaka kanisani hatuna hata mbuni;
hakuna madawati watoto wanakaa chini mashuleni;
sare zao zimetoboka matakoni;
wabunge wao wanasinzia tu bungeni..
new model land cruiser wan_z_paki tu uwani;
sisi wametuacha kwenye mataa haliduni;
wanaishi zao tu mijini tuvyoishi ni kama mateka tu vitani;
hakuna madawa hospitalini bima ya afya akupe nani?;
majisafi hayatoki mabombani;
hawachimbi visima eti umekauka mto wami;
siku hizi hakuna bunge live kideoni;
huu mwaka wa ishirini bado mnatuahidi mtaweka lami;
lawama tumpe nani?
wanapitisha tu kokeni mateja wan_z_di tu kujaa mitaani;
magendo yanapita tu bandarini hatupo hata makini;
wanasafirisha makinikia watuambia sio madini;
ndege zinatua wanyama wanaibiwa tu porini;
nyie kopeni cag anatuambia yanaongezeka tu madeni;
nduguzao wanawateuwa wapo wilayani madaraka yashawalevya kwani mtawafanya kitu gani;
wanaharakati na watetezi wote wapojela wanakesi za uhaini;
waliponea chupuchupu walikimbilia uhamishoni;
ukizungumzia katiba mpya wanakutia tu mbaroni;
hii ni ndoto nimeiota mchana kweupe wala sio jioni;
كلمات أغنية عشوائية
- рома желудь roma zhelud › рома желудь (roma zhelud) – киберпанк (cyberpunk) كلمات اغاني
- dtf › dtf – pas d’câlin كلمات اغاني
- halogic › halogic – manar l’falsafa كلمات اغاني
- jah9 › jah9 – intention كلمات اغاني
- replus › re:plus – headline كلمات اغاني
- duncan sheik › duncan sheik – summer mourning كلمات اغاني
- cam james › cam james – my god freestyle (future – perky’s callin’ remix) كلمات اغاني
- tank › tank – slp2 كلمات اغاني
- jasko › jasko – dreckskanakke كلمات اغاني
- andrew bayer › andrew bayer – tomorrow boys كلمات اغاني