kalimah.top
a b c d e f g h i j k l m n o p q r s t u v w x y z 0 1 2 3 4 5 6 7 8 9 #

dizasta vina – wachezaji wa timu كلمات اغاني

Loading...

wanasema duniani kuzimu
kwanini ukeshe kushika protocol wakati
ulaji muhimu
watu wanachohifadhi ni mbinu
kucheza kulia kushoto ila wote ila wote
ni wachezaji wa timu

chumba kilijaa njemba za kisasi
walipanga vifaa ka’ wanakwenda kwenye kazi
palikuwa jitu juu meza yenye glass
limeshika tissue kusafisha chemba ya risasi

walijaa na maninja na ma bouncer
wamevimba wenye sura za kutisha
wamekausha
wamegadhibika mpaka amani ilijificha
nilihisi mkojo unatiririka kwenye trouser

sura za kutisha nafuu devils
crate zimemwaguka utadhani sikukuu kesho
kulikuwa k_mejaa camera full angles
huku warembo waki_twerk twerk juu ya pool table

huku watemi wa ngenga wameketi
mwonekano wa rostam bakhrеsa na mengi
palikuwa na mabegi ya cheda na chеnchi
yalikuwa mengi hata wachache kubeba hawawezi
walikuwepo mabinti wamefanya line up
mfano wa dinner set sura ziko innocent
zikionyesha zina majuto ya kusign up
na baadhi yao walikuwa wadogo yaani minors

babake jesca alisimama kwenye chanja
ametingwa kuchanganya plama kwenye ganja
nikamsalimia hakuijibu salamu yangu
akavuta beri kisha akapiga chafya mara saba

kabla muda wake wa k_maliza
akanyonga jani akapaka mate kwenye lizzla
akasnap vidole kuonyesha alikuwa taita
k_mwita mrembo na mrembo akaja na lighter

mrembo akamwashia kipuri wakapiga puff mbili
wakatoa moshi wakaanza kukiss pasi siri
ka’ wacheza ngono mbele ya binti yake jesca na mbele yangu kiasi nafsi ikakosa tafsiri

baba’ake aka_struggle kuk_mbuka jina langu
nikamwambia jina langu naitwa toni glove
akauliza umemjua vipi binti yangu
nikamwambia mi na jesca tumekutana kwenye coffee shop

akaisogelea glass, akanywa kilich0m_ kisha
aka_scan majibu
ili kuhakikisha ninachokiongea fact, akasema sikujui unatokea wapi
nikamwambia nimezaliwa hapa nonde sua
nyumba no 77 kwa mzee kilua.akasema ninapiga simu mbili tatu kama hawakujui
nitakushauri tu uombe dua

akaja mtu akani_snap kwenye iphone
design kama anafanya michongo ya passport
akainua uso nikaona umeweka ndita
akatikisa kichwa kisha akaendelea ku_type more

mkono wa jesca begani ukinipeti peti
huku moyo w_ngu ukienda lesi lesi
board guard wake wakinichekicheki
mara wani_search mif_ko mara wani_search begi

nikaletewa maji ili nipoze kiu
design hamu ilinikata mzee
wasaidizi wakingiza jina langu kwenye simu ya kimtandao
kunifanyia background check

babake jesca
akanipa face look kisha
akaomba simu sikubisha
akaanza kukagua photo akalog in kwenye social kunikagua facebook twitter

ghafla ukimya ukaitawala nyumba
wakati akili ikiwaza kufa
nikitushwa na yale mandhari yanayofanana na nyumba ya mafia mkubwa
kutoka kuala lumpur
akauliza je nipige down town
maana najua kila mtu kule ukinidanganya bure
nitakukausha kama kau kau mpaka uta shout shout
jesca akasema daddy calm down

mi na tony tayari tumependana
amekuja kutoa mahari ili tuishi ka’ mke na bwana
anaomba kibali anataka kunioa
na kama utakubali basi soon tutafunga ndoa

baba jesca akaegemea kwenye kiti mwisho
akashusha pumzi kwa masikitiko
kwanini unadate na mtu hatumjui
na unajua style ya kuleta hawa wakati ringi
mwiko

jesca unajua hadhi ya hii business
equation ya ndoa haifiti into this case
kwanini usitafute a guy from inside
ipo time utaleta ma_spy au ma_witness

jesca akajibu daddy tony doctor
phd holder chuo kikuu cha oxford
anamiliki migahawa kadhaa hapa town
_n_lipwa vizuri na kipato kinamtosha

namfahamu tony sio mnoko
na kwao wana uwezo sana baba yake don sio kitoto
tumejuana miaka kadhaa ameshanikaa
maana penzi nililolihifadhi moyoni sio kidogo

babake jesca akanicheki amenuna
nikawa nimevex nimechuna
moyo unaenda resi kama duma
mabaunsa yapo next yametuna
yakisubiri mechi hii kubuma

nikamwona mshikaji ameshika panga bisu
alikuwa busy anapanga vitu
sura yake ilikuwa tayari kuanza bifu
jesca akaniambia yule kaka’angu na ana anger issues

akaja ameshika vipisi vya kete
kisha akanidadisi si kibwege
akashout naskia harufu ya polisi kwa huyu bwege
jesca akamuwahi akasema we’ chizi acha usenge

akatoa syringe kwenye small bag
akauliza unapendaga cocaine
nikamwambia huwa situmii hizo zaga
kaka’angu alitumia akabwaga akajibu okay

nilihisi harufu ya casket
kaka’ake jesca alihisi mi’ shushushu akani_suspect
nikahisi napokwenda sio
moyo w_ngu ukienda mbio

babake jesca nae anahamaki
baada ya kugundua nina camera kwenye kifungo cha shati
akatoa bunduki nikahisi uhai w_ngu unaishia
ndipo polisi wenzangu wakavamia

كلمات أغنية عشوائية

اهم الاغاني لهذا الاسبوع

Loading...