kalimah.top
a b c d e f g h i j k l m n o p q r s t u v w x y z 0 1 2 3 4 5 6 7 8 9 #

kerly d - asante lyrics

Loading...

karibu kwenye kituo cha mabasi
yaendayo haraka maarufu kama mwendokasi
tunanunua pesa mbovu, pesa za kigeni
na pesa zozote ulizokuwa nazo, mimi nanunua

alhamdulillah, asante mungu
alhamdulillah, asante mungu

aah, it is a new day
karibu mtaani kwetu
mtaa wa bora liende
usiulize eee
haya ndiyo maisha yetu
tunapamba kombe

awe tunashukuru tunacho kipata
kiwe kidogo ama kikubwa
ahsante baba, aah
na tunaridhika maana tamaa huzaa ubaya

eeh, me ndiyo msomi pekee kwa familia yetu
ajira hakuna, nipo ninashona viatu
siwezi kusikia maneno ya watu
wakati kichwa changu kimejaa madeni tupu

ukiniona napambana eeeh
usidhurumu haki yangu
nilipotoka kuna noma eeh
anaejua yote mungu
ila watu tumetoka mbali mbali sana
aah, watu tumetoka mbali mbali sana

hapa tulipo tunasema
alhamdulillah, eeeh asante mungu
tulichopata tunasema
alhamdulillah, baba baba, asante mungu
hapa tulipo tunasema
alhamdulillah, eeeh asante mungu
na tukikosa tunasema
alhamdulillah, baba baba, asante mungu

yeah, from zero to hero
asubuhi nimeamka, nipo doro
mchana nimepata jero
asante mungu
yeah
kila hatua kuna dua
sio mpaka nipate kikubwa
hata kwa hiki kidogo
asante mungu

eeh, me sijui mboga saba
wala pizza baga
ili mradi unanipa kushiba
asante mungu
jana ilikuwa kusudi
leo kama zawadi
ntazidi fanya juhudi
asante mungu

awee eeeh
kuna watu wanachukulia powa
juhudi zetu wanafanya mtaji
w_ngejua jinsi tunavyoumia
sie ndiyo tunatafuta ulaji
eeeh, me ndiyo mlezi pekee wa familia yetu
nategemewa kuleta chochote kitu
napiga kazi kutwa mchana na usiku
halafu kuna watu wanabana nisi tusu

ukiniona napambana eeeh
usidhurumu haki yangu
nilipotoka kuna noma eeh
anaejua yote mungu

ila watu tumetoka mbali mbali sana
aah, watu tumetoka mbali mbali sana

hapa tulipo tunasema
alhamdulillah, eeeh asante mungu
tulichopata tunasema
alhamdulillah, baba baba, asante mungu
hapa tulipo tunasema
alhamdulillah, eeeh asante mungu
na tukikosa tunasema
alhamdulillah, baba baba, asante mungu
alhamdulillah aaaaaaaa
alhamdulillah aaaaaaa
baba babaaaa
uuuuuuuh

كلمات أغنية عشوائية

اهم الاغاني لهذا الاسبوع

Loading...